Mimi ni mzaliwa wa Kenya ambaye amekuwa akizungumza Kiswahili tangu utotoni. Ninakukaribisha kwa moyo mkunjufu kujifunza Kiswahili pamoja nami. Nitakusaidia kuzungumza kwa ufasaha katika muda mchache iwezekanavyo.
Ninawasaidia wanafunzi wanaohitaji msaada katika: kuzungumza Kiswahili kwa ufasaha, kuandika katika lugha ya Kiswahili au kupita mitihani ya Kiswahili. Mimi ni mwenye urafiki hivo nina uhakika kuwa utafurahia kujifunza lugha hii pamoja nami.
Mimi ni mwenye urafiki na mwenye subira. Ikiwa una maswali yoyote sitasita kuyajibu. Nitatarajia mwanafunzi awe makini na mwenye bidii. Kwa kushirikiana pamoja nawe sina shaka lolote kwamba utabobea katika lugha hii :)